BUMACO YANG’ARA KWENYE UZINDUZI WA KIJIJI CHA BIMA

BUMACO YANG’ARA KWENYE UZINDUZI WA KIJIJI CHA BIMA

  • Date 04-07-2025

Kampuni za Bumaco Insurance Co. Ltd na Bumaco Life Insurance zimeshiriki kikamilifu katika Uzinduzi wa Kijiji cha Bima, uliofanyika siku ya Ijumaa, tarehe 4 Julai 2025, katika Viwanja vya Saba Saba – Kijiji cha Bima, kuanzia saa 3:30 asubuhi hadi 5:30 asubuhi.

Tukio hilo la kitaifa limehudhuriwa na wadau mbalimbali wa sekta ya bima nchini, likiongozwa na Kamishna wa Bima Tanzania, Dkt. Baghayo Saqware, ambaye alitoa hotuba ya uzinduzi akisisitiza umuhimu wa elimu ya bima kwa wananchi na nafasi ya sekta hiyo katika kukuza uchumi.

Kupitia banda lao maalum, Bumaco ilitoa elimu kwa wananchi kuhusu huduma mbalimbali za bima.

Ushiriki wa Bumaco katika tukio hili ni ushahidi wa dhati wa dhamira yao ya kuendelea kusogeza huduma karibu na wananchi, kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa bima, na kuchangia katika ujenzi wa jamii yenye kinga ya kifedha dhidi ya majanga.